Huddah: Nimechoka na maisha ya Kenya

huddah-monroeNAIROBI, KENYA
MREMBO maarufu nchini Kenya, Huddah Monroe, ameweka wazi kwamba amechoka na maisha ya nchini humo kutokana na kuzushiwa mambo anayodai yanaharibu jina lake.
Mwanamitindo huyo amedai hata anapojaribu kuwa kimya kwa muda mrefu baadhi ya watu humchokoza kupitia mitandao ya kijamii.
“Niliamua kuwa kimya kwa muda mrefu, lakini bado kuna watu wananitafuta kwenye mitandao ya kijamii na kuweka habari zisizonihusu, hii hali inaniumiza sana na inanipa wakati mgumu.
“Kuna wakati nafikia hatua kwamba nikimbie nchi yangu kutokana na habari za kunishambulia kila siku, mimi ni binadamu kushambuliwa mara kwa mara najisikia vibaya, naomba kila mmoja afanye mambo yake,” aliandika kwenye akaunti yake ya Twitter Huddah.
Previous
Next Post »